Burudani

Instagram waifungia akaunti ya Idris Sultan, aeleza kilichosababisha

Instagram imeifungia akaunti ya mshindi wa BBA 2014, Idris Sultan.

T3-The-winner-of-the-ninth-season-of-Big-Brother-Africa-themed-Big-Brother-Hotshots-Idris-Sultan-Pic-Major-moves-Comedy

Idris ameimbia Bongo5 kuwa hatua hiyo imekuja baada ya kuvunja masharti ya mtandao huo.

Amesema anadhani sababu za kufungikiwa kwa akaunti yake ni kutokana na kupost kipande cha video kutoka kwenye filamu ya The Interview iliyowahi kupigwa marafuku katika baadhi ya nchi.

“Nafikiria labda kutokana na ile part, ndio kitu pekee kilichosababisha kwasababu hakuna ukiukwaji mwingine wowote niliofanya,” amesema.

Idris amesema kitu pekee kinachoweza kusababisha mtu kufungiwa akaunti ya mtu bila taarifa ni pale anapoweka picha za utupu ama kama mtumiaji mwingine ametoa malalamiko kuhusu akaunti husika.

Anasema kwa sasa kila anapotaka kuingia kwenye akaunti hiyo anaambiwa ‘you account has been disabled.’

Hata hivyo amesema mchakato wa kuirejesha unaendelea na anaamini ndani ya wiki moja itakuwa imereja. Instagram wamewahi kuifungia akaunti ya Rihanna baada ya mrembo huyo kupost picha za utupu.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents