Bongo Movie

Irene Uwoya atangaza vita na Flora Mvungi


Vita vya maneno kati ya waigizaji wa filamu nchini Flora Mvungi na Irene Uwoya jana vimechukua sura mpya.
Wiki iliyopita tuliandika habari kuhusiana na Flora kutofurahishwa na kitendo cha Irene kuongea na vyombo vya habari na kusambaza shutuma kuwa mpenzi wake wa zamani H.Baba hajui mapenzi.
Jana Irene Uwoya aliongea na Clouds Fm na kusema Flora na H.Baba wamemchokoza.
Alisema yeye pia anamshangaa Flora kwa kupakaza maneno kuwa aliongea na magazeti ‘kumvua nguo mpenzi wake wa zamani H’Baba kuwa ni zezeta kitandani kitu ambacho alikanusha kukisema.
Irene alisema kwanza anamuona Flora ni mshamba na kumfananisha na ‘vocha’ na kamwe sio saizi yake.
Aliongeza kuwa yeye si mtu wa kutembea na H.Baba na kudai kuwa wako pamoja na Flora kwakuwa wote ni washamba na wote amewafananisha na vocha.
‘Sasa leo nasema kuwa kweli H.Baba hajui mapenzi, hana lolote, ni tegemezi na simtaki,alisema.
Akiongea kwa jaziba, Irene aliongeza kuwa yeye yupo level zingine na anawadharau wapenzi hao.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents