Ivan bado anampenda mno Zari, asema mpambe wake (Picha)
Anaishi maisha ya kifahari, ni tajiri, anamiliki magari ya gharama kubwa, ana mijengo, biashara kibao na ana uwezo wa kumpata msichana yoyote anayemtaka kwa kutumia nguvu ya utajiri wake, lakini Ivan bado hajamsahau Zari the Bosslady aliyezaa naye watoto watatu wa kiume.
Kwa mujibu wa mpambe wa King Lawrenc, Ivan ambaye ni raia wa Uganda anayeishi nchini Afrika Kusini, hajaweza kukubali matokeo kuwa Zari kwa sasa yupo mikononi mwa Diamond Platnumz.
Ivan
Lawrenc anaamini kuwa Ivan bado hajampata au kumwona msichana mwingine mrembo zaidi ama kama Zari ili awe kusonga mbele na maisha yake.
Lawrenc amepata msichana wa kizungu nchini humo aitwaye Miss Rose na anaamini kuwa kama Ivan akipata msichana kama huyo ndipo atakapoweza kumsahau Zari ambaye kwa sasa ana mtoto na Diamond.
Miss Rose
“I think if @ivandon can find a beautiful gal like @therealmissrose, then he can move on from @zarithebosslady,” aliandika Lawrenc kwenye picha ya mrembo huyo aliyoiweka kwenye Instagram.
Ivan pia amekuwa akitumia akaunti yake kuwataka followers wake wamemfollow mrembo huyo.