Burudani

Izzo Bizness aeleza kinachokwamisha collabo ya The Amazing na Ycee

Mwaka jana mkali kutoka Nigeria,Ycee alidondoka Bongo na kufanya ziara kwenye media mbalimbali kwa lengo la kutangaza muziki wake na kukutana na baadhi ya wabongo Fleva.

Miongoni mwa vitu alivyovifanya akiwa nchini, ni kolabo ambayo aliifanya na kundi la The Amazing, taarifa ambayo ilithibitishwa na Izzo Bizness.

Ni muda sasa umepita na hakuna taarifa yoyote juu ya collabo hiyo.

Kupitia kipindi cha Supermega cha Kings Fm,Izzo ameweka wazi sababu za kuchelewa kwa ngoma hiyo. Izzo Amedai kuwa target yao ilikuwa ni kutoa video pamoja na audio, lakini wamepata ugumu kumpata Ycee ili kushoot video,suala ambalo limefanya washindwe kutoa ngoma hiyo mapema.

Pia amedai hawawezi kutoa audio pekee kwani sio lengo lao.

Prince Ramalove
Kings Fm

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents