Burudani
Izzo Bizness awashirikisha Fid Q, Jay Moe na Shaa kwenye ngoma mpya ‘Inanichosha’
Rapper na mjasiriamali wa Mbeya, Izzo Bizness anatarajia kuachia wimbo mpya uitwao ‘Inanichosha’ aliowashirikisha Fid Q, Jay Moe na Shaa.
Akiongea na Times FM, Izzo B amesema mdundo wa wimbo huo umetayarishwa na producer KTB wa Mbeya na kisha vocal na mixing zimefanywa na Master Jay.
“Kuna vitu tumeongea tu ambavyo vipo vinaendelea katika maisha, katika hii game ambavyo vinachosha, yaani kwamba habari fulani na hali fulani inayoendelea inachosha, unajua. Nafikiri ikitoka watu ndo wataelewa nini ambacho namaanisha zaidi kwa sababu utamu hatuwezi kuumaliza sasa hivi,”amesema Izzo.