Burudani
J.Cole atangaza kuachia albamu ya tano Ijumaa hii
J. Cole is back. Msanii huyo anatarajia kuachia albamu yake ya tano Ijumaa hii ya April 20.
Rapper huyo amethibitisha hilo kupitia mtandao wa Twitter na kutaja jina la albamu hiyo itaitwa ‘KOD’.
“New album. KOD 4/20,” ameandika Cole kwenye mtandao huo.
Cole amewahi kuachia albamu nyingine nne ikiwemo ‘Cole World: The Sideline Story’ (2011), ‘Born Sinner’ (2013), ‘2014 Forest Hills Drive’ (2014), 4 Your Eyez Only (2016).