Burudani

Jacqueline Wolper amcharukia vikali Madee

Muigizaji wa filamu Bongo, Jacqueline Wolper amempa onyo kali msanii wa muziki Madee kwa kumtengenea katuni ambayo imeonekana katika video mpya ya masanii huyo bila makubaliano.

Kupitia amtandao wa Instagram Wolper ameandika maneno yanayoashiria kukerwa na kitendo hicho na kumtaka msanii huyo awasiliana naye endapo atahitaji kufanya biashara hiyo.

Embu ona jamani macho natia huruma kama na upwiro kilo 200 …hii mikaka yetu yakibongo kuna mida inaboa kuna mida inakuwa powa ..sasa Madee Rais wamnzese nikuulize swali…ulishindwa nini kunyanyua ka cm kako nakunipgia ata kinafk nakunambia unanivdio queen katuni sjui sanam unajua wewe….acha dharau wewe pumbavu piga cm omba kwanza….ata kma umlipi m2 sisi tunasaidiana wote wasanii leo kwangu kesho kwako,??. nakunishika kimahaba umenishika una dhambi wewe kaka na suit umenivalia kma unaenda kutoa posa kwa masawe?..sasa onyooo siku nyingne ombaga utapewa acha kuparamia kama vile unaomba round kwa kimada wako kwanza unitafute utoe ata faini ya kuniweka macho kama nimevuta ugoro…ila nyimbo kali nisiwe mchoyo nanimependa idea ila mwambie alinichonga nakunipa hyo shepu nitampasua ?

Madee alitumia sura ya Wolper katika video yake mpya ‘Sikila’ ambayo amemshirikisha Tekno kutoka nchini Nigeria. Itazame hapa chini.

Na Laila Sued

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents