Habari

Jaguar awasalimu kwa picha hii! yenye passport, UK pound za kutosha, saa za gharama, simu bila kusahau pakti ya condom

Ulikuwa bado una wasiwasi na utajiri wa msanii wa Kenya Jaguar? Well, sio mimi ni yeye ndio katoa tip ya kile alichokuwa amebebea jana jioni kabla ya kupanda ndege kurudi nchini Kenya akitokea UK.

Jaguar

Katika picha aliyoiweka kulikuwa na Passport yake ili wasije kusema alitumia picha ya mtu mwingine, then cheni moja ya gold ya hatari, saa mbili za gharama, Samsung Galaxy note, Calvin Klein Cologne na noti za UK pound za kutosha.

Lakini Jaguar amedhihirisha hana kigeugeu katika swala zima la kujilinda, alikuwa na pakti moja ya condom aina ya durex, nadhani hii ndio iliyobaki, LOL!.

Hit maker wa ‘Kigeugeu’ Jaguar alikuwa akirejea Kenya baada ya kuvuka boda kama alivyoimba katika wimbo wake ‘Navuka boarder’ akitokea London Uingereza ambako alitumbuiza katika show moja na TID wa Tanzania.

Picha na ghafla Kenya.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents