Jay Z amfagilia Obama
Nyota wa Muziki wa Hip hop duniani Jigga Jay Z hivi karibuni alifanya bonge la Show jijini New York, lakini kali kuliko zote ni pale Jigga aliposikika hadharani akiongea maneno yaliyowapa picha mashabiki kuwa anamfagilia bwana Barack Obama
Nyota wa Muziki wa Hip hop duniani Jigga Sean Carter Jay Z hivi karibuni alifanya bonge la Show jijini New York akiwa na mshikaji wake Mary J Blige, inasemekana kwamba kila aliyehudhuria alionekana kuvutuiwa na kumuona akiwa sambamba na Blige jukwaani.
Lakini kali kuliko zote ni pale Jigga aliposikika hadharani akiongea maneno yaliyowapa picha mashabiki waliokuwepo katika onesho hilo kuwa anamfagilia mgombea wa kiti cha uraisi wa Marekani bwana Barack Obama na kumdisi live Raisi wan chi hiyo mheshimiwa George W. Bush.
Jigga alisikika akiwauliza mashabiki waliokuwemo katika ukumbi huku akirudia mara kwa mara mko tayari kwa mabadiliko pia aliweka wazi na kutaka ieleweke kuwa onesho hilo halihusiani na kudhaminiwa na mgombea huyo wa kiti cha uraisi Bwana Barack Obama kwa ajili ya kampeni.
Minongono ya utani ilisikika ikisema kuwa iwapo Obama atashinda katika kinyanganyiro hicho upo uwezekano kwa Jay Z akakosa cha kurap.