Burudani
Jay-Z na Beyonce ndio couple ya kwanza kwenye muziki kuwa bilionea
Kwa mujibu wa International Business Times, Shawn Carter & Beyonce Knowles Carter ni couple ya kwanza kwenye muziki yenye utajiri wa pamoja wa dola bilioni moja.
Beyonce anatarajia kukusanya zaidi ya dola milioni 116 kwenye ziara yake, Mrs. Carter World Tour. Ukiongezea na zile dola milioni 50 za kampeni ya Pepsi na kampeni H&M, amesaidia kuongezea fedha za familia na ‘billion dollar mark’ mwaka huu.
Kwa upande wa Jay-Z tayari ni namba mbili kwenye orodha ya FORBES richest Hip Hop artists akipata fedha nyingi kutoka kwenye makampuni yake ya muziki, urembo na timu za mpira.