Siasa
Jay Z na Will Smith waungana na Obama kuhusu ndoa za jinsia moja
Jay-Z na Will Smith wameunga mkono tamko la Barack Obama kukubali ndoa za jinsia moja nchini Marekani, tamko ambalo lilipokelewa kwa hisia tofauti nchini kwa na kwengine duniani.
Will Smith alisifia tamko la Obama kuwa ni la kijasiri katika mwaka wa uchaguzi nchini Marekani, na aliendelea kusema kwamba ni jambo la kuunga mkono mtu yoyote akipata mwenzake wa kuwapenda na kuwasaidiana katika maisha.
Kwa upande wake Jigga alisema anaamini kuwa wapenzi wa jinsia moja wanapaswa kuwa na haki ya kuoana, na kwamba kinachofanyika majumbani mwao si suala lao wenyewe.