Burudani

JB adai alizitolea nje ofa tatu za movie Kinaijeria

JB si msanii anayezuzuka na filamu za Kinaijeria ndio maana amesema ameshazitolea nje ofa tatu za kuigiza filamu za Kinaijeria.

13249723_626702900838700_2108717596_n

“Natoboa siri ambayo watu hawaijui, nimekataa script zaidi ya tatu Nigeria kwenda kuact kwasababu hazinilipi,” muigizaji huyo aliiambia 255 kupitia kipindi cha XXL cha Clouds FM.

“Naapa mbele ya Mungu ukitaka nitakuonesha, zipo. Sababu ni moja tu fedha iliyolipwa ni ndogo wakisema kwamba tunakutengeneza ili wakujue. Siko tayari kutengenezwa sasa hivi, mimi ninachotaka ni hela. Filamu yangu moja hapa nikiuza napata hela nzuri sana,” ameongeza.

JB amesema international anayoitaka yeye si kwenda kufanya filamu Nigeria bali kutengeneza filamu ambayo itaoneshwa kwenye majumba ya sinema duniani.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents