Burudani

JB ana mchango mkubwa kwenye kipaji changu – Kajala Masanja

Msanii wa filamu Kajala Masanja amesema haikuwa kazi rahisi kwake kufika hapo alipofikia bila ya mchango wa msanii mkubwa wa filamu nchini, Jacob Stephan aka JB.
kajala

Muigizaji huyo ambaye ni miongoni mwa wasanii wanaowania Tuzo za EATV 2016, alishare siri ya mafanikio yake mbele ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Kampasi ya Mlimani), huku wakiwataka wanafunzi hao kuuliza baadhi ya maswali.

Akizungumza na wanafunzi hao, Kajala alisema yeye hakupata changamoto kubwa katika kupata nafasi ya kuonyesha uwezo wake.

“Mimi namshukuru JB, ndiye aliyenisaidia mpaka nikafika hapa,” alisema Kajala. “Lakini moja kati ya changamoto ambazo nilizipata wakati naanza nilikuwa nataka kufanya filamu na watu wakubwa kitu ambacho kilikuwa hakiwezekani kwa wakati ule, lakini mwisho wa siku nilivumilia mpaka nikapata nafasi,”

Muigizaji huyo anawania tuzo ya muigizaji bora wa kike katika tuzo za EATV Award 2016.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents