Jd kuwa Dj
Mkongwe wa filamu nchini Jacob Steven ‘Jb’ anatarajia kuwakutanisha waigizaji wawili Wema Sepetu na Irene Uwoya katika filamu yake mpya ya Dj Ben, ambayo anatarajia kuiachia Desemba mwaka huu.
Akizungumzia filamu hiyo alisema kwamba kwamba, itazungumzia maisha ya wanandoa ambao wanafanyaa kazi nchi mbili tofauti, na matatizo yanayowakuta wakiwa mbali hususani kwenye suala zima la Mapenzi.
Amesema pia Irene na Wema wamekuwa wakishindana kuhusiana na mwigizaji bora, mwanzo Irene aliibuka na ushindi lakini kwa mara ya pili akaibuka Wema, lakini kwenye filamu hiyo wote watakuwepo.
Aliongeza kwa kusema kwamba pia kuna filamu inayokuja kwaajili ya kuwashindanisha wasanii hao wawili, ambayo nayo ipo jikoni yaja. Jb alisema katika filamu hiyo yeye ndiye atakuwa Dj.