Burudani
Je Halle Berry ni mjamzito?
Msindi wa tuzo za Oscar Halle Berry mwenye miaka 50 amezua taharuki katika mitandao baada ya kuonekana akiwa anakitumbo kinachoashiria kuwa ni mjamzito.
Halle Berry
Berry mwenye watoto wawili alizua taharuki hiyo wakati wa red carpet ya 16th Annual Chrysalis Butterfly Ball jijini Los Angeles -Marekani ambapo kamera za wapiga picha zilimnasa mama huto akiwa na kitumbo hicho.
Muigizaji huyo nguli ambaye mwaka jana Desemba aliachana na mumewe Olivier Martinez, wiki iliyopita alipost katika ukurasa wake wa Instagrama kuwa ‘No more boyfriends’.
Berry amezua maswali katika mitandao ikiwemo je nani baba wa mtoto huyo ajae au ni ameshiba tu chakula?.
Na Laila Sued