Burudani

Je, ni kweli Alikiba anafanyiwa fitna kwenye muziki wa Bongo Fleva? Mwenyewe atoa majibu haya (+Video)

Baada ya malalamiko kuwa msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Alikiba anafanyiwa figisu figisu kwenye muziki wake jambo ambalo linamfanya apate tabu kusonga mbele na kufanikiwa, Hatimaye msanii huyo kafunguka ukweli wa jambo hilo.

Alikiba

Alikiba akiongea na Bongo5, Amesema kuwa yeye kama mkongwe kwenye gemu hafanyiwi figisu figisu zozote zile na yanayoendelea hayana ukweli wowote ule.

Alikiba amesema “Siamini kama kuna michezo hiyo,” na kuwataka mashabiki waendelee kutoa sapoti kwa kazi zake na za wasanii wa Kings Music ambapo amesema kuwa kuanzia sasa itakuwa ni mwendo wa kuachia ngoma juu ya ngoma.

 

 

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents