Burudani
Je! Wajua? Sijutii ya Joh Makini ilirekodiwa mwaka 2007!!
Wakati mwingine nyimbo mpya tunazozisikiliza redioni huwa mpya kwenye masikio yetu tu lakini zimerekodiwa muda mrefu mno. Unaweza kuamini kuwa ngoma ya Joh Makini iitwayo Sijutii ilirekodiwa mwaka 2007?
Kwa maana nyingine ni kuwa ngoma hiyo ambayo video yake ilitoka mwezi uliopita ilirekodiwa miaka sita iliyopita. Audio ya wimbo huo imeanza kusambazwa rasmi leo, December 27.