Je zama za Mourinho kutua Madrid zimefika ?, zaidi ya viti 30, 000 vyakosa watu Santiago Bernabeu usiku wa jana
Zaidi ya viti alfu 30, 000 vilikosa mashabiki kwenye dimba la Santiago Bernabeu hapo jana siku ya Jumapili na kuwa habari kubwa ya msimu.
Hali hiyo imetokea wakati Real Madrid wakikubali kipigo cha mabao 2 – 0 dhidi ya Real Sociedad huku wakiachwa kwa tofauti ya alama 10 mbele ya vinara wa ligi Barcelona.
Meneja wa timu hiyo, Santiago Solari amepoteza imani ya kujiamini kwa zaidi ya miezi kadhaa sasa huku akiwataka wachezaji wake kuhakikisha wanafanya jambo litakalo saidia kuwarudisha mashabiki wao uwanjani kama ilivyokuwa hapo awali.
Cristiano Ronaldo aliiwezesha miamba hiyo ya soka ya Hispania kutinga hatua ya fainali ya UEFA Champions League na kutwaa ubingwa huo Ukraine. Na kuwapiga mabingwa wa Japan ambapo walichukua taji jingine kitu ambacho mpaka sasa Ramos au Solari wanaonekana kutoweza kufikia hatua hiyo.
Mpaka sasa kunamjadala wapengine, Mourinho kuchukua kazi hiyo katika kipindi hiki ambacho Barcelona wanaongoza kwenye msimamo wa La Liga huku nyota wake, Lionel Messi na Luis Suarez wakishindana kupachika mabao.
Katika kipindi hiki Madrid italazimika kununua wachezaji ili kuweza kuhakikisha wanajikwamua kutoka hapo ilipo.
Miamba hiyo ya soka ya Hispania ilishindwa kumnunua Eden Hazard dirisha la usajili lililopita baada ya kuandaa kitita chafedha kwaajili ya kumnyakuwa Neymar mwaka huu 2019, huku kukiwa na siri kuwa Marco Asensio na Isco wanachangia katika kuhamasisha nyota huyo wa PSG anafanikisha kutua.