Michezo

Jerry Muro ateuliwa kuwa msemaji mpya wa Yanga

Mtangazaji wa zamani wa vituo vya ITV na TBC1, Jerry Muro ameteuliwa kuwa msemaji mpya wa club ya Yanga.

muro
Jerry Muro

Kwa mujibu wa gazeti la Mwanaspoti, Muro anachukua nafasi ya Baraka Kizuguto ambaye sasa atakuwa meneja wa timu hiyo. Gazeti hilo limedai kuwa uamuzi huo wa Yanga ulitolewa katika kikao kilichofanyika Jumapili hii.

Chanzo kimoja kimeliambia gazeti hilo kuwa mkataba wa Kizuguto ulikuwa unakwenda ukingoni na hivyo wameamua kutomwongezea mkataba.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents