Burudani

Jibu la Chin Bees kuhusu kusambaza picha za ‘kimahaba’ ili kupata kiki

Msanii wa muziki Bongo, Chin Bees amefunguka undani wa picha ambayo imesambaa mtandaoni ikimuonyesha akiwa katika mahaba na mrembo ambaye bado hajafahamika.

Muimbaji huyo ameiambia E-Newz ya EATV kuwa picha hiyo imesambaa mara baada ya simu yake kupotea ambayo ilikuwa na hizo picha.

“Kwa hiyo mimi ni mtoto wa kiume vitu kama vile nafanya lakini siyo kufanya public, mimi siyo mtu wa kiki na wote wanaomjua Chin Bees siyo mtu wa style hiyo,” amesema.

Alipoulizwa iwapo huyo ndiye mpenzi wake, alijibu, “Siyo official, ingekuwa official ningesema ila tulikuwa katika namna gani zile ndio ikatokea picha hizo lakini namshukuru Mungu watu wangu wameweza kunielewa kwa sababu mimi siyo mtu style hiyo,”.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents