Burudani

Jibu la Irene Uwoya kuhusu Dogo Janja kuoa mke wa pili

Mke wa msanii wa muziki Dogo Janja, Irene Uwoya ametoa majibu juu ya habari zilizopo za mumuwe kutaka kuongeza mke wa pili hadi wanne.

Uwoya ametoa majibu hayo baada ya kukuta habari zimezagaa katika mitandao mbalimbali juu ya mpingo ya mumuwe aliyoweka ya kutaka kufikisha idadi ya wake wanne katika ndoa.

“Ndoutajua mim Kabila gani…thubutu uwone tena wasikudanganye @dogojanjatz,” ameandika mrembo huyo katika mtandao wake wa kijamii wa Instagram mapema leo baada ya kuona stori za mumuewe za kumuongezea mke zikitawala.

Katika kipindi cha The Playlist ya Times Fm kilichoruka juzi ( 12-03-2018) mkali huyo wa ‘Wayu Wayu’ alidai kuwa anampango wa kuongeza mke wa pili hadi wanne kila baada ya miaka 10.

Soma zaidi: Baada ya Irene Uwoya, Dogo Janja kuongeza mke wa pili.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents