BurudaniLady Jay Dee
Jide na Kidumu kufanya Party ya tuzo zao
Lady Jay Deeanatarajia kufanya party maalum ya kujipongeza yeye pamoja na Kidumu, katika mgahawa wake NyumbaniLouge ulipo Namanga . Anasema katika party hiyo pia utakuwa uzinduzi maalum wa siku ya jumapili ambayo atakuwa akipiga show, yeye mwenyewe kwa kupiga nyimbo ake pekee.
Kiingilio katika party hiyo ya aina yake ni shilingi 30,000 kama mambo ya msosi yatakuwa juu yao, lakini shilingi 20,000 kama masuala ya msosi utajitegemea kwa kununua mwenyewe.
Na kuanzia siku hiyo na kila jumapili Jay Dee atakuwa akitumbuiza yeye mwenyewe katika jukwaa hilo la Nyumbani Louge.
Anawaomba mkaribie kwani kutakuwa na burudani moto moto na mambo mazuri.