Michezo
Jina la Bafana Bafana kufutwa??!!
Timu ya soka ya Afrika ya Kusini imejikuta kutishiwa kuachana na jina la Bafana Bafana kufuatia utata wa kisheria wa haki miliki. Chama cha soka cha Afrika ya Kusini [SAFA] kinavutana na mfanya biashara mmoja ambaye alinunua hakimiliki ya jina hilo mwaka 1994.Wamiliki wa sasa wa jina hilo walitengeneza paundi millioni 10 wakati za fainali zilizo pita za kombe la Dunia.
Rais wa SAFA Kirten Nemetandani alisema jina hilo sasa litajadiliwa kitaifa kwa nia ya kuachana nalo kutokana na mzozo huo wa kibiashara uliojitokeza.