Burudani
Joh Makini na Davido hawajaamua nani atamiliki wimbo watakaofanya
Joh Makini amesema bado yupo kwenye mazungumzo na Davido ili kujua nani atakuwa mmiliki wa wimbo watakaofanya au kama utakuwa unamilikiwa na wote.
Rapper huyo amesema ikifika wakati ataweka wazi kila kinachoendelea kwenye kazi hiyo inayosubiriwa kwa hamu.
“Ni mapema zaidi kujadili wimbo utakuwa ni wa kwake au wa kwangu hadi kila kitu kitakapokamilika ramsi. Kwa sababu bado tupo kwenye mazungumzo ya kujadili ni wa kwake au wa kwangu au wa wote,” Joh Makini aliambia XXL ya Clouds FM.