Burudani
John Legend na mkewe Chrissy Teigen wapata mtoto wa pili
John Legend na mke wake, Chrissy Teigen wamepata mtoto wao wa pili ambaye anadaiwa ni wakiume.
Wawili hao wamedaiwa kupata mtoto huyo Alhamisi hii baada ya Chrissy kuandika ujumbe kwenye mtandao wa Twitter ambao unaonyesha familia yao kwa sasa imeongezeka.
“Somebody’s herrrrrrre! 🍼🤗🍼🤗,” ameandika Chrissy kwenye mtandao huo.
Wawili hao walipata mtoto wao wa kwanza, Luna Simone Stephens mwezi April 2016.