Jokate mbioni kuolewa
Aliyekuwa Miss Tanzania namba mbili mwaka 2006 na mwanamitindo kwa sasa, Jokate Mwegelo ameeleza kuwa yupo mbioni kuolewa.
Mwanamitindo huyo ambaye anatamba na brand ya Kidoti ametumia ukurasa wake wa mtandao wa Instagram kueleza hilo hata hivyo hakumtaja muhusika.
jokatemwegelo March Baby 👼🏽. March Queen 👸🏽👩🏽💻👩🏽🍳. Soon to be somebody’s Wife 👰🏽and Mummy🤰🏽. God is Great and Faithful. Grown but forever a baby girl 🤗😘. Ni kwa neema tu na rehema.
Ujumbe huo unakuja ikiwa leo ni siku ya kuzaliwa kwa mrembo huyo ambaye pia amesikika na kuonekana katika video kadhaa za muziki wa Bongo Flava.
Soma Pia;Napenda nipate watoto mapacha – Jokate
June mwaka jana katika mahojiano na Gazeti la Mtazania Jokate alisema anatamani umri ukifika apate watoto mapacha na wote awalee katika maisha ya kijijini na mjini ili wajue maisha ya pande zote mbili na kuweza kujifunza kilimo na kula chakula vya asili.