Awards
Jokate Mwegelo ndio official host wa red carpet ya KTMA
Mtangazaji wa Channel O, Tanzania, Jokate Mwegelo atakuwa host wa red carpet kwenye tuzo za muziki za Kilimanjaro Tanzania, KTMA Jumamosi hii, June 8. Tuzo hizo zitafanyika kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.
Shughuli nzima itaanza saa 1 jioni ambapo itaoneshwa live kwenye mtandao kuanzia muda huo.
Pia mtangazaji wa kipindi cha Power Jams cha East Africa Radio, Sam Misago amepangwa kuwa mwendesha shughuli (host) wa socia media lounge.
Baada ya red carpet Sam na Jokate wataungana pamoja ambapo watakuwa wakiwahoji wasanii baada ya kupokea tuzo.