Michezo
Jonjo Shelvey ajiunga na Newcastle United
Klabu ya soka ya Newcastle uUited imemsajili kiungo Jonjo Shelvey kutoka Swansea City.
Newcastle, wamelipa kiasi cha pauni milioni 12 kumsajili kiungo huyu wa kimataifa wa Uingereza mwenye umri wa 23.
Jonjo alifanikiwa vipimo vya afya na amesaini mkataba wa miaka mitano na nusu kukitumikia kikosi hicho cha Steve Mclaren.
Baada ya uhamisho huo kukamilika kocha mkuu wa kikosi cha Newcastle alimzungumzia mchezaji huyu na kusema, “Ni mchezaji mwenye uzoefu katika viungo wa kati wa kiingereza.”
Hata Hivyo timu ya zamani ya Jonjo, Charlton,watapata kiasi cha mgao wa mchezaji huyo aliyeng’ara kama kiungo wa klabu ya Swansea msimu huu.