Habari

Jose Chameleone amdondoshea mke wake Daniella party ya nguvu kwenye birthday yake

Beautiful Daniella akiwa na mwanae

Kubali au kataa, Jose Chameleone ni miongoni mwa wasanii wa Afrika Mashariki wenye wake warembo zaidi. Haipiti wiki hajamtaja kwenye ukurasa wake wa Facebook na hakika kwa urembo huo wa Daniella, mzee wa Valuvalu ana haki ya kudata.

Jana ilikuwa ni birthday ya mke wake huyo aliyezaa naye watoto watatu na aliamua kumwangushia party ya nguvu kwenye kisiwa chake cha Leone.

“Happy birthday my darling wife Daniella Atim Mayanja. May you live to blow a million candles. Fans and Leone island family u are invited to the pary today! @ berbeque lounge centenary park starting 8pm, leone island tugende tukole,” aliandika.
Tunajiuliza amempa zawadi gani awamu hii!

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents