Burudani
Jose Chameleone apanga kuhamia Kenya
Muimbaji wa Uganda, Jose Chameleone ana mipango ya kuhamia nchini Kenya.
Chameleone amedai sababu za kutaka kuhamia Kenya ni kutokana na jinsi vyombo vya habari vya Uganda vinavyomwandika vibaya.
Amedai kuwa amefikia sehemu ambayo amechoka kuandikwa kwa mambo mabaya kuliko mazuri na kwamba Kenya ni sehemu anayoipenda na kuichukulia kama nyumbani.