Jose Mourinho aanika mambo matatu yanayoitafuna Manchester United, akiri Paul Pogba kuchangia kuachishwa kazi
Jose Mourinho amesema kuwa matatizo yanayoisumbua klabu ya Manchester United yapo kwa wachezaji, mfumo na malengo huku akimtaja mchezaji, Paul Pogba kuwa anahusika kwa kuachishwa kwake kazi.
Mourinho ambaye alikuwa kocha Mkuu ndani ya timu hiyo ya Man United, alitimuliwa kazi mwezi Desemba, wakati matatizo ya mahusiano yake dhidi ya Pogba yalianza mwezi Septemba hadi kupelekea kupewa kitambaa cha unahodha ili kuweka mambo sawa ndani ya uwanja ingawaje haikuwa kama ilivyotarajiwa.
Alipoulizwa kama alikuwa ameathiriwa na Pogba, Mreno huyo aliliambia gazeti maarufu la michezo nchini Ufaransa L’Equipe “Hapana, matatizo yapo pale, unaweza kuwamini kuwa matatizo ni wachezaji, mfumo na malengo.”
“Nitaweza kusema tu kwamba, siwezi kusema ndiyo, uliponiuliza kama Paul Pogba ni yeye tu anayewajibika.” Mourinho amesema hayo wakati alipoulizwa anadhani Pual Pogba ndiyo chanzo.
Ole Gunnar Solskjaer alichukuliwa kiziba nafasi ya Mourinho kwa kupewa mkataba wa miaka mitatu baada ya kuitumikia United kama kocha wa muda huku akishinda mechi 14 kati ya 19 alizoisimamia United na kuisaidi kurudi ‘top four’.
Lakini hata hivyo kuonekana timu hiyo ya Manchester United kumshinda baada kushindwa kusalia kwenye ‘top four’ na kushika nafasi ya sita huku ikipokea vipigo.