Michezo
Jose Mourinho aongea kuhusu kurudi katika soka
Baada ya kukaa kimya tangu aachishwe kazi, kocha wa zamani wa klabu ya Chelsea, Jose Mourinho ametoa kauli yake mpya baada ya kutokuwa tayari kuzungumzia soka katika kipindi chote hicho.
Mourinho ambaye anahusishwa na kujiunga na Man United ili kuchukua nafasi ya Louis van Gaal, amesema yupo tayari kurejea hivi karibuni licha ya kuwa wengine wanamtafsiri kama mjeuri, lakini yeye anasema ni mtu wa kawaida na anajifunza popote.
“Siku zote nimekuwa nikijifunza hata katika sehemu ambayo najihisi ni mtaalam, siku zote mimi sio mkamilifu na nimekuwa nikijifunza kila siku, wakati mwingine katika kazi na hata maisha binafsi,” alisema.
“Narudi karibuni katika soka sehemu ambayo nahisi ni maisha yangu ya asili.”