Michezo
Jose Mourinho asema hakuna bora kama yeye
Kocha wa Chelsea, Jose Mourinho amesisitiza kuwa yeye ni bora kushinda yeyote yule katika kuifunza klabu hiyo licha kupoteza mechi tatu mfululizo katika msimu huu.
Baada ya kichapo hicho cha mabao 3-1 dhidi ya Everton ,Mourinho alisema kuwa watu wengi sasa wanafurahia janga lake. “Haya ni matokeo mabaya zaidi katika kazi yangu,” alisema Mourinho. “Sijazoea mambo kama haya lakini sasa nimeanza kuyaelewa katika kazi yangu.Hata hivyo sihisi shinikizo yoyote,”aliongeza.
“Mimi ndiye ninayefaa kwa kazi hii, sidhani kama kuna mtu zaidi yangu anayeweza kuifanya kazi hii.”