Joshua amuongoza Hamilton tuzo ya mwanamichezo bora wa mwaka 2017
Bingwa wa uzito wa juu duniani, Anthony Joshua anaongoza katika orodha ya wachezaji 12 waliyotangazwa kuwania tuzo ya mwanamichezo bora wa mwaka 2017 nchini Uingereza kupitia shirika la BBC.
Bingwa wa uzito wa juu duniani, Anthony Joshua
Joshua mwenye umri wa miaka 28, ambae ni bingwa wazamani wa Olympic na bingwa wa uzito wa juu amekuwa akipendwa zaidi tangu alipotwaa taji lake la WBA na IBO baada ya kumshinda mpinzani wake Wladimir Klitschko katika dimba la Wembley mwezi Aprili.
Huku bondia huyo akifanikiwa kuutetea mkanda wake wa IBF katika pambano lake la hivi karibuni dhidi ya Carlos Takam mwezi Oktoba katika Uwanja wa Cardiff Principality uliyojaza mashabiki 80,000.
Anthony Joshua anakabiliana na ushindani mkubwa kutoka kwa bingwa wa mwaka 2014, Lewis Hamilton ambae pia ni mshindi mara nne wa mashindano ya Formula One mwezi uliyopita na Chris Froome mshindi mara nne wa mashindano ya Tour de France.
Dereva wa mashindano ya Formula One, Lewis Hamilton
Mwanariadha, Mo Farah mshindi wa mbio za dunia mita 10,000 jijini London huku katika listi hiyo akiwemo mchezaji wa Tottenham, Harry Kane.
Kane ni mfungaji bora wa ligi ya Uingereza mwaka 2016/17 na kuisaidia Uingereza kufuzu michuano ya kombe la dunia.
Mchezaji tenis namba moja kwa ubora nchini Uingereza, Johanna Konta nimiongoni mwa wachezaji waliyotangazwa katika listi ya kuwania kinyang’anyiro hicho.
Mwendesha baiskeli, Chris Froome mshindi mara nne wa Tour de France
Mo Farah, bingwa wa dunia wa mbio za mita 10,000 jijini London
Harry Kane, mfungaji bora wa ligi kuu nchini Uingereza mwaka 2016-17
Mchezaji tenis namba moja kwa viwango vya ubora nchini Uingereza, Jo Konta
Mchezaji wa michezo ya katika barafu, Elise Christie
Jonathan Rea,
Mwanariadha, Jonnie Peacock
Muogeleaji, Adam Peaty
Mchezaji kriketi mwanadada, Anya Shrubsole bingwa wadunia
Bianca Walkden (kulia), bingwa wadunia wa mchezo wa taekwondo