Burudani
Jukwaa la shindano la Miss Bumbum 2018 lageuka uwanja wa ndondi Brazil, mshindi ashambuliwa na wenzake (+video)
Jukwaa la Shindano la Miss Bumbum 2018 nchini Brazil, limegeuka ukumbi wa masumbwi baada ya majaji kumtangaza, Mrembo Ellen Santana kuwa mshindi wa shindano hilo.
Bi. Ellen alivuliwa taji hilo na mshiriki mwenzake, Aline Uva ambaye alikaririwa akisema kuwa majaji wamempendelea kwani makalio yake ni bandia hakustahili.
Shindano la Miss Bum Bum ni moja ya mashindano makubwa nchini Brazil, na linahusisha wanawake wenye makalio makubwa kama kigezo cha kushiriki. Tazama video hapa chini