Burudani

Juma Nature: Nikitaka ubunge wa Temeke naupata kirahisi kabisa

Juma Nature anaamini kuwa akiamua kugombe ubunge wa Temeke ataupata kirahisi.

10747764_1557908607756732_1472941098_n

Nature ameiambia XXL ya Clouds FM kuwa alishafuatwa na baadhi ya viongozi wamkita agombee nafasi hiyo.

“Walishanifuata watu, lakini kwa mwaka huu nimeona kwanza nikaushe,” amesema Nature. “Mimi mbona ubunge wa Temeke nakula, tena vizuri kabisa, bila hata matatizo. Kwa vyama mbalimbali siwezi kuvitaja, nimeacha kwanza akina Professor wachukue kwanza, lakini baadaye miaka mingapi usije ukashangaa nipo mjengoni, nimevaa suti kali,” aliongeza msanii huyo.

Nature alisema akiwa mbunge wa Temeke ataanza kushungulia miundo mbinu ya barabara pamoja na ujenzi holela ambao umekuwa ukisababisha mafuriko mara kwa mara.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents