Burudani

Jux ataja muda wa kumaliza masomo yake China

Mashabiki wa Juma Jux, wamekuwa na swali gumu ambalo wamekuwa wakijiuliza na kukosa majibu kuhusu kikomo cha masomo cha Msanii Jux nchini China.

Muimbaji huyo amefunguka kupitia kipindi cha Vmix cha Channel Ten kuwa, ifikapo mwezi wa sita mwaka huu ndio utakuwa mwisho wake wa masomo nchini humo.

“Nimekuwa nikisoma kwa muda mrefu nchini China na safari zilikuwa nyingi sana hapa kati mara kwenda kurudi kwenda tena kurudi. Ninachoshukuru ni kuwa hazijawahi kunifelisha kwa sababu nimekuwa mpangaji mzuri wa ratiba za masomo, muziki na maswala yangu binafsi. Kwa hiyo Mungu kabariki na mwezi wa sita mwaka huu namaliza masomo nchini china,” amesema.

Hitmaker huyo wa Umenikamata, amewataka mashabiki kusubiria vitu vizuri kutoka kwa kundi lao la Wakacha na kuongeza kuwa haliwezi kufa kwa kuwa wao ni kama familia.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents