Burudani

Jux ‘feki’ azua balaa Njombe

Mtu aliyejitambulisha kama Jux ambaye ni muimbaji amekuwa tishio katika mkoa wa Njombe baada ya kutapeli kiasi cha shilingi laki tatu za Promota na nyingine za wafanyabiashara wa nguo.

Wakati wakazi wa mji wa Makambako, Njombe wakimsubiri kwa hamu kubwa Jux siku ya Jumapili kwenye show ambayo ilitangazwa itafanyika katika Ukumbi wa Mid Town, muandaaji wa show hiyo amejikuta katika wakati mgumu baada ya kufanyiwa utapeli huo.

Kupitia Kipindi cha Zero Planet ya Ice FM ya Njombe, Promota huyo anayefahamika kama Sele, amesema, “Huyo jamaa nishawasiliana naye na nishampa kama laki tatu ya hela yake ikawa imebaki kama laki moja hivi. Hata jana usiku amenipigia anasema mimi nataka nijiandae nije kesho ila akasema niongeze laki mbili ili aje na Ben.” Alipoulizwa kwanini alimuamini huyo jamaa kwa kiasi hicho Sele anasema yeye alimuamini kupitia picha ya WhatsApp.

Wakati huo huo mtangazaji huyo alipomtafuta Jux ‘Original’ alikataa kuwa na show wikiendi hii mkoani humo siku hiyo kwa kusema, “Huo ni uongo sina show yeyote Njombe inawezekana hao ni matapeli tu. Yaani mimi ndio nasikia kwako pia sina show kokote.”

Baada ya kupata majibu ya Jux mwenyewe ilibidi kumtafuta huyo ‘Jux Feki’ nakufanya nae mazungumzo, nayo yalikuwa kama hivi:

Jux Feki: Nambie
Gami: Poa Poa Jux mida hii wapi mwanangu

Jux Feki: Dah mwanangu nipo barabarani.
Gami Dee: Jux hee kunataarifa nimepata unashow unakuja kufanya Makambako Njombe huku imekaaje?

Jux Feki: Enheee ndio hiyo hiyo na kuja Juma Pili
Gami Dee: Unakuja na nani?

Jux Feki: Nakuja na Ben.
Gami Dee: Utakua na Ben Pol?

Jux Feki: Ndio
Gami Dee: Sasa unawaambia nini mashabiki zako pande hizi Jux?

Jux Feki: Enhe hehe he yaani sina cha zaidi zaidi ya kuwaambia kuwa nitatoa T-shirt mbili watu watatu kuwahi kuingia ukumbini.

Gami Dee: Unamipango ya kuachia ngoma hivi karibuni manaake kama kimya?
Jux Feki: Soon Kitawaka.

Gami Dee: Unaachia ngoma gani na umefanya na producer gani?
Jux Feki: Hiyo siri mjomba siri hiyo mjomb

Gami Dee: Na video mbele au hapa hapa bongo?
Jux Feki: aaaaaah video uwani mbele kidogo nyuma kidogo

Gami Dee: Sijakuelew?
Jux Feki: Yaani nje kidogo ndani kidogo

Gami Dee: Yaani umechanganya location saizi?
Jux Feki: enheee

Gami Dee: Ameshuti Justin Compos au umesafiri na director?
Jux Feki: aaaaah director?

Gami Dee: nasema director aliekutengenezea ni Justin au umeenda na director kutoka bongo?
Jux Feki: niii hiyo ni Nje nje

Gami Dee: sasa mwanangu mi nipo Ice Fm Makambako na nimeongea na Jux Original Jux anasema hana taarifa za kuja kufanya show makambako ndio maana nikakucheki wewe we ni Jux gani mzee?

Jux Feki: we umeongea wa wapi huyo?
Gami Dee: Nimeongea na Jux mwenyewe nimetoka kuongea nae sio muda

Jux Feki: Hapana
Gami Dee: na kaniambia hana show yeyote Njombe kwanini umeamua kutumia jina la Jux kutengeneza mkwanja hali we sio

Jux mzee?
Jux Feki: Hapana sio kweli

Gami Dee: Inaonesha hata wakati huu nawataja madirector wa South Africa anaofanya nao kazi Jux huwafaham?
Jux Feki: Sio kweli

Gami Dee: Kunadirector gani wa South Africa anayefanya kazi na Jux we unamfahamu?
Jux Feki: asee badae badae utanipigia baadae.

IMEANDIKWA NA: @gamideetz
+255 715971027

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents