Habari
Kairuki akanusha tetesi kuwa serikali itaanza kuhakiki watumishi wa umma wanavyotumia mishahara yao
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Angela Kairuki amekanusha tetesi kuwa serikali itaanza kuhakiki watumishi wa umma wanavyotumia mishahara yao.
Amelazimika kuzikanusha taarifa alizoziita za uongo kupitia akaunti yake ya Twitter.
“Kuna taarifa ya uongo inayosambazwa mtandaoni kwamba “kutakuwa na zoezi la kuhakiki watumishi wa umma wanavyotumia mishahara yao, Ipuuzieni,” ameandika.
“Si dhamira wala desturi ya Serikali yetu kuingilia maisha binafsi ya watumishi wa umma hususan matumizi ya mishahara yao.Puuzieni uzushi huo,” ameongeza.