Burudani
Kalapina aanzisha harakati Afrika
Mwanamuziki kutoka kikundi cha muziki cha Kikosi cha Mizinga kilichopo Kinondoni block one, Karapina amesema kwa sasa yupo kwenye harakati za kutangaza amani Afrika kwa kutumia muziki wa Hip Hop akiwa na mwanamuziki mwenzake Suma rago.
Amesema Tour hiyo ameanzia Dar es salaam kisha akaja, South Africa katika miji ya Port Elizaberth, Cape Town, Pretrolia. Anasema baada ya hapo anatarajia kuzunguka miji mingine ya Afrika na hata nje kama akipata nafasi hiyo.
Karapina anadai kwamba huko kote kuna wadau wake wa Kikosi ambao ndiyo wanaompa Support ya kufanya hizo show. Pia akasema kwamba katika Show zake zote, huwa anauza T-shet na Cd za albamu zao, ambazo huwa zina lipa sana kwenye mauzo kama hayo…..