Burudani
Kalapina adai ‘Good Time’ aliyomshirikisha Ommy Dimpoz imemuongezea mashabiki wa kike
Msanii nguli wa Hip hop hapa Bongo, Kalapina amesema anaona ngoma yake mpya ya ‘Good Time’ aliyomshirikisha Ommy Dimpoz imemletea mashabiki wapya wa kike.
Kalapina amesema hayo wakati akiongea na ENews ya EATV.
“Unajua kwa muda mrefu sikuwa nimehusisha ngoma ya mapenzi katika kazi zangu ila baada ya kuamua kufanya kazi ya aina hiyo na kumshirikisha mwana Bongo Flava, Ommy Dimpoz, naweza kusema kuwa rekodi hii imekuwa ni ngoma ya hip hop inayochezwa na pia kununuliwa mtandaoni zaidi.”