Michezo

Kama hutaki Ole Gunnar aendelea kuinoa Manchester United hilo sahau, atoa siri nzito ya mikakati yake na mkurugenzi Ed Woodward kuisuka timu upya



Kocha wa Manchester United Mnorway, Ole Gunnar Solskjaer amefunka wazi kuhusu kile alichomwambia Ed Woodwar kuhusu malengo ya klabu yake.

Akiongea hayo baada ya kumalizika tukio la kutia saini beki wa timu hiyo Phil Jones na kusema:- “Lakini maamuzi, wakati mwingine wa hatima ya wachezaji haupo chini yangu, pia ni wachezaji wenyewe, wanataka kukaa, wanataka kuendelea, wanataka kitu kingine?

“Tuna maono na picha ya jinsi gani tunataka kuiandaa katika miaka michache, tunapaswa kufikiria muda mrefu lakini pia muda mfupi .. Nina picha ya jinsi nadhani timu hii ya Man Utd itaonekana katika miaka michache.”

“Sijui ikiwa ni pamoja nami, lakini mara zote ninaweka maoni yangu kwa Ed Woodward na wale walio kwenye klabu.”

Alipoulizwa kama mtazamo wake ulibadilika tangu alipofika, aliongeza: “Sio kweli nimeiunga mkono United kwa miaka mingi tangu nilikwenda nyumbani.Na nilikuwa na mtazamo wa wazi juu ya maono yangu kuwa namna itakavyokuwa”

“Unapata mtazamo tofauti wa wachezaji wengine: ‘amevutiwa na mimi, na anatamani tuendelee”

“Sisi hatujatofautiana sana na hatuko mbali sana na kile nilichofikiri wakati nilipofika hapa Manchester United nikiwa kama kocha.”

By Ally Juma.



Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents