Habari
Kamati Kuu ya CCM yatoa siku 7, Membe, Kinana na Makamba
Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM), imetoa siku 7 kwa kamati ya Usalama na Maadili ya chama hicho kukamilisha taarifa ya mahojiano juu ya wanachama watatu, Yusuph Makamba, Abdulrahman Kinana na Bernard Membe na kuiwasilisha katika vikao husika.