Michezo

Kamati ya Nidhamu yamwachia huru mwingine aliyefungiwa na TFF

Kamati ya Rufaa ya Nidhamu ya TFF, imeendelea kuwatoa kifungoni wadau mbalimbali ambao waliokuwa wamefungiwa kutojihusisha na soka.

Damas Ndumbaro ambaye ni wakili na wakala wa wachezaji ambaye miaka mitatu iliyopita alifungiwa kutojihusisha na soka kwa kipindi cha miaka saba ameachiwa huru.

Ndumbaro ni mtu wa pili kuachiwa na kamati hiyo baada ya hapo juzi mkuu wa kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Simba, Haji Manara kuachiwa huru kutoka kwenye kifungo alichopewa cha kutojihusisha na soka kwa kipindi cha mwaka mmoja.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents