Habari

Kamishna wa tume ya uchaguzi Kenya IEBC aachia ngazi

Kamishna wa Tume ya Uchaguzi Roselyn Akombe ajiuzulu, asema tume imegawanyika na inafanya kazi bila kuzingatia utaratibu.

Dr. Akombe alituma taarifa kutoka New York alipokuwa akifanya kazi Umoja wa Mataifa kabla ya kwenda kufanya kazi tume ya uchaguzi

Katika taarifa hiyo Dr. Akombe alisema uchaguzi uliopangwa kufanyika hauwezi kukidhi matakwa ya uchaguzi unaoaminika

” Kwa jinsi tume ilivyo sasa ni hakika haiwezi kutuhakikishia uchaguzi utakaoaminika tarehe 26 Oktoba. Sitaki kuwa sehemu ya dhihaka hiyo kwa uchaguzi wa kiadilifu”

Akihojiwa na shirikala utangazaji la BBC Jumatano Asubuhi, amesema amekimbilia New York akihofia usalama wa maisha yake na pia na kuongezea Mwenyekiti wa Tume hiyo, Wafula Chebukati amezingirwa

Alikuwa ni sehemu ya timu iliyokuwa isafiri kwenda Dubai kusimamia kuchapishwa kwa karatasi za uchaguzi

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents