Habari

Kampuni ya SBL yamtangaza Mark Ocitti kuwa mkurugenzi mpya

Kampuni inayoongoza kwa uzalishaji wa bia nchini, Serengeti Breweries Limited (SBL) imemteua Mark Ocitti kuwa Mkurugenzi Mtendaji mpya kuchukua nafasi ya Helene Weesie anayeondoka.

Helene amekuwa na SBL kwa miaka minne kuanzia mwaka 2015, kipindi ambacho kampuni imeweza kuzindua bidhaa muhimu zilizosababisha ukuaji wa biashara kwa kiasi kikubwa ikiwa ni pamoja na kampuni kupata tuzo za ubunifu na kuongezeka kwa uwekezaji.

Helene anaondoka kwenda kuchukua nafasi nyingine ndani ya Diageo barani Ulaya. Akiwa nchini Tanzania atakumbukwa, bali na mambo mengine, kwa kuibua na kuendeleza vipaji vya ndani ya nchi.

Mkurugenzi mtendaji mpya, Mark Ocitti, kwa sasa anahudumu katika nafasi sawa na hiyo katika kampuni ya Uganda Breweries Limited (UBL) ambayo pia ni sehemu ya kampuni mama ya East Africa Breweries Limited (EABL) inayoongoza kwa uzalishaji wa
vinywaji katika ukanda wa Afrika Mashariki.

Ocitti, chini ya uongozi wake, UBL imeweza kupiga hatua kubwa katika
utendaji wake na kupelekea kukua kwa biashara.

Akizungumzia uteuzi wa Ocitti, Mkurugenzi Mtendaji na Afisa Mtendaji Mkuu wa EABL, Andrew Cowan amesema: “Mark amefanya mageuzi makubwa katika biashara yetu nchini Uganda; ameongeza nafasi yetu kiushindani na kukuza faida ya UBL kwa kipindi cha miaka mitatu iliyopita.

“Sina shaka kwamba kutokana na uzoefu wa uongozi wa Mark, maono, pamoja na mipango mikakati yake shupavu, itaifanya biashara ya SBL, inayokua kwa kasi kukua hata zaidi.”

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents