Michezo

”Kamwe siwezi kuifundisha Tottenham, nawapenda sana mashabiki wa Chelsea”-Kauli ya Mourinho 2015, je ni nini kimembadili ?

Jose Mourinho amekuwa kocha mpya wa Tottenham licha ya kuwa mwaka 2015 aliwahi kusikika akisema kuwa kamwe hatakuwa mwalimu wa timu hiyo kutokana na heshima yake kwa Chelsea.

Four years later, Mourinho has now replaced Mauricio Pochettino as manager of Tottenham

Mreno huyo ambaye amewahi kuifundisha Chelsea na kuipatia mataji mawili hatimaye amechaguliwa kuwa kocha mpya wa wapinzani hao wa London hapo jana siku ya Jumanne kufuatia kufukuzwa kazi kwa Mauricio Pochettino.

Wakati wa fainali ya ‘League Cup’, mwaka 2015 Chelsea ikiikabili Tottenham kwenye dimba la Wembley, Mourinho amesema amekuwa akihitajiwa Mwanyekiti wa Spurs, Daniel Levy ili kuyabeba majukumu ya White Hart Lane mwezi Septemba 2007.

Mourinho made the comment shortly before Chelsea beat Spurs to win the 2015 League Cup

Na ndipo, Mourinho amesema 2015 kwamba kamwe hatokuwa kocha wa Tottenham, hii ni kutokana na hisia zake kwa Chelsea.

Lakini pia ameafikiana na Chelsea kwamba hatokuja kufundisha klabu nyingine za Uingereza kwa miaka miwili ijayo baada ya kuja kuachana na The Blues.

Image result for 'I could NEVER manage Tottenham... I love Chelsea fans too much!' Mourinho insisted in 2015 that he rejected Spurs in 2007... so what's changed, Jose?

Alipoulizwa kuwa aliwahi kuhitajiwa na Spurs mwaka 2007, Mourinho alisema ni kweli ”Ni kweli, lakini sikuenda, wala sikuwa na klabu nyingine hapa Uingereza kwa muda wa miaka miwili. Sikuchukua kazi yoyote kwa sababu ya kuwapenda mashabiki wa Chelsea.” Mourinho ameipatia Chelsea mataji matatu ya Premier League, FA Cup na matatu ya League Cups.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents