Kanye West abezwa kwa nguo alizodesign
Rapper turned Designer wa nguo, Kanye West, ameambulia patupu baada ya kupondwa kwa nguo alizodesign na kuonyesha kwa wadau wa mitindo na mavazi mjini London.
Inasemsekana mavazi hayo, amabayo aliyadesign kwa kile kinachosadikika kua pesa nyingi,zilikua kama vile zimetengenezwa na mtoto mdogo.
Mwandishi mmoja wa gazeti la NY Times,amesema nguo za Kanye zilikua hazieleweki na bora akae tu kwenye sanaa ya Hip Hop kabla hajatinga kudesign nguo.
Mr. West aliwajibu critics wake kwa jazba kama kawa, na kusema kwamba walikua hawamuelewi na pia hawaielewi fashion na mapinduzi anayojaribu kuyaleta kwenye industry hiyo ya fashion.
Alisema ni kitu ambacho anapenda kufanya tangu akiwa kijana na anajua kwamba yeye ni mkali kwenye design.
Mdau unaonaje haya mavazi?