Burudani

Kanye West afuta akaunti yake ya Instagram na Twitter, sababu za kiakili na kisiasa zatajwa

Rapper Kanye West kwa mara nyingine amefuta akaunti zake za mitandao ya kijamii ya Twitter na Instagram, hii ni baada ya kushambuliwa vikali mitandaoni na mashabiki wake kuhusu msimamo wa kumsifia Rais Trump.

Related image
Kanye West

Kanye West japokuwa hajatoa sababu ya kujiondoa mitandaoni, lakini vyombo vya habari nchini Marekani vinaeleza kuwa alikuwa kwenye kipindi kigumu mitandaoni baada ya kuweka wazi hisia zake kuwa anamsapoti Trump.

SOMA ZAIDI – Kanye West abadili jina, adai Marekani ya Trump imekuwa mkombozi kwa vijana

Jumamosi ya wiki iliyopita, Kanye West akiwa kwenye kipindi cha Saturday Night Live kinachorushwa na kituo cha NBC alikaririwa akiusifia uongozi wa Trump huku akiwa amevalia kofia iliyoandikwa ‘Make American Great Again’ kauli mbiu inayotumiwa na Rais Trump.

Nimeongea na watu wengi weupe wananiuliza kwanini unampenda Trump? ile hali ni mbaguzi?..mimi nawajibu angekuwa mbaguzi watu wote weusi tungehama Marekani tukaishi nchi nyingine.“alisema Kanye West kwenye mahojiano hayo huku mamia ya watu waliokuwa kwenye tukio hilo wakimzomea na wachache wakipiga makofi.

Baada ya kumaliza kipindi hicho cha SNL, Kanye akaamua abadilishe jina na kujiita YE na leo usiku ameamua kufuta kabisa akaunti ya Twitter na Instagram.

Matatizo ya msongo wa mawazo na kushindwa kuhimili mashambulizi kutoka kwa mashabiki wake, yalimpelekea Kanye West mwaka jana kufuta akaunti zake za mitandao ya kijamii.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents