BurudaniUncategorized
Kanye West amuimbia shabiki wake kabla ya mauti kumkuta
Kanye West alifanya ndoto ya shabiki wake kuwa kweli hivi karibuni, kwa kumpigia simu na kumuimbia muda mfupi kabla ya kufa kwa kansa.
Kazi nzuri aliyo ifanya Kanye isingejulikana kama isingekuwa mtumiaji wa Twitter aitwaye Debbie, ambaye alitweet
“Msichana huyu ambaye naishi naye mtaa mmoja alikuwa na kansa na Kanye alimpigia siku mbili zilizopita na kumuimbia ” alisema. “Nadhani Kim alikuwepo pia. Haikutambuliwa hata na vyombo vya habari vya kijamii au chochote. Nina heshima sana kwa yeye, kwa kumfanya afurahi wakati wake wa mwisho. ”
Tweets by stalkdebbie
Kim Kardashian alionekana kuwa amethibitisha tukio hilo kwa kujibu “Tunasali kwa ajili ya familia yake.”
Na Raheem Rajuu